Kuongelea Taaluma usiyoijua na hasa kama hii, kidogo mtu unapaswa kuwa jasiri, ama chizi kabisa kama alivyoasa mwalimu Nyerere juu ya kugusa mambo ambayo wengi wamekwisha yafanyia kazi na kuamua tofauti na unavyodhani. Na watanzania ni wepesi wa kumchukia
mtu anapoonekana kuwa muongo,Tanki linaomba watanzania wasilichukie kama huu pia ni uongo kwa sababu katika maisha, mara nyingi kuelewa ni kugumu kuliko kutafsiri, hivyo maana inaweza kueleweka kitaalamu na kikawaida na ama vinginevyo. Tanki, linawakilisha uelewo wa vinginevyo kama mbongo, na hivyo kutoa nafasi kwa wataalamu kutoa mwanga zaidi na sahihi katika mjadala huu muhimu kwa taifa letu. Architecture (A) ni Taaluma ya usanifu wa ujenzi, kimsingi kwa Tanzania