ONDOA BORA ELIMU WEKA ELIMU
BORA MAMBO YAKIMBIE
According
to The Education Act of 2002(2)(1) of
Tanzania, “Education means the instruction or training of people of all ages in
various fields of learning designed to contribute to the spiritual,moral,mental
and physical development of the community and the attainment of the wider
national goals”.
Kwa ujumla tu kwetu sisi Watz, kwa sheria yetu
wenyewe, nafikiri ya kiswahili pia ipo,ni uvivu tu wa kuitafuta! Maana ya Elimu
ni maelekezo or mafunzo wanayopatiwa watu katika marika tofauti na nyanja
mbalimbali yaliyosanifu kuweza kutoa mchango wa maendeleo Kiroho,Kiutu,Kifikra
na Kifizikia/muonekano wa kisura katika jamii na kufanikisha kufikia malengo ya
Taifa kwa mapana yake! UBORA ELIMU HUO, Kwa nini kiswahili iwe shida kwa
Mtanzania? Kama hatuwezi kubadili tulichosoma kutoka lugha tuliyotumia kusoma
kwenda kwenye lugha yetu, ni vipi tuweze kunufaika kama jamii na elimu hiyo
tuliyoipata kupitia lugha hiyo! Ah nafikiri inawezekana!
Tayari kujigonga huku,
Utasikia huyu Yanga kaanza na Njano
na Nyeusi! Mwingine huyu atakuwa Simba mbona Nyekundu na Nyeupe ndio kubwa!
Hadi Ba Rizi najua atajiuliza tu kimoyomoyo!
Tukiachana na Utani huo wa jadi,
Muelekeo wa elimu yetu sio mzuri, hasa kwa upande wa ubora. Ripoti
mbalimbali zinaonyesha hilo,na sio tu sisi bali na wenzetu nchi za
jirani,lakini hayatuhusu sana huko!Tokea muda
mrefu suala la elimu bora limekuwa likiongelewa na wadau mbalimbali, lakini haina maana
haliwezi kuongelewa leo! Na kufuatia ombi la President’s Office, Planning and Commission (POPC),kuchangia maoni juu ya suala hili, Tanki nalo limo!
Usibishe kabla hujasoma, utamaduni
wetu mbaya kabisa ni kutosoma! Wanasema UKITAKA KUMFICHA KITU MTANZANIA, WEKA KWENYE
MAANDISHI! Pengine ndio
chanzo cha makosa kwenye kuingia mikataba mbalimbali, na kupenda kuongea
Saana kuliko kutenda. Na may be, I think, Inawezekena, Unajua,Inabidi na mungu
akipenda , nyingi! kwenye kila kitu!
Soma Mdau! Acha utamaduni mbovu wa kukimbia maandishi!
According to the[(World
Bank. (2000), Higher Education in Developing Countries: Peril and Promise.
Washington D.C: The world Bank.]report, of all levels Higher Learning Instutions provide fertile
grounds for cross-pollination of representatives of all disciplines into a
single place .It stressed that, developing countries can hardly benefit from the global knowledgebased economy,unless
the Quantitative
effort being made, get the help of qualitative
effort and in relevance to local
conditions.
Mpaka sasa ni miaka zaidi ya kumi! Kama Hatuja pata
suluhu ya Ubora wa Elimu,inaashiria kuchelelwa,lakini Chelewa ufike, ah hapana,
msemo mzuri hapa ni Heri Nusu Shari Kuliko Shari Kamili!
Hiyo ni ripoti ya Benki ya Dunia iliyoandikwa mwaka 2000,
ndio,tafiti tunafanyiwa kwa sababu zetu hata kwanza ngumu sana, proposal
ipite upewe hela, weee! Na tukifanya kwa hela zetu kimtindo, atazisoma nani kwa
kupitia wapi wakati hazina sifa! Unataka kusifiwa,wakati za profesa wako
hazijapita,zimewekwa kando zinasubiri budget ijayo,na ndio maana wakati
mwingine zinawanufaisha watu wa mbali kabisa!
HATA KAMA RESEARCH YAKO YA ‘KATI YA
MVUA NA JUA BORA NINI?’ HAINA PROPOSAL,TUTAISOMA TUONE
ULICHOTUFUNZA AU MAPUNGUFU ULIONAYO,ILI TUJUE TUKUSAIDIAJE!
Ripoti hii YA
BENKI YA DUNIA ilionesha wazi kuwa bila jitihada za dhati kupandisha UBORA WA ELIMU,HASA VYUO VIKUU,AMBAMO WANAKUTANISHWA
WATU KUTOKA MAENEO MBALIMBALI NA WANAOTEGEMEWA KWENDA KUTUMIKIA TAIFA KATIKA
NYANJA MBALIMBALI, BASI NCHI ZINAZOENDELEA ZISAHAU KUNUFAIKA KWA LOLOTE KATIKA
DUNIA YA UTANDAWAZI.
Actually,
University Education as a key representative must be excellently
fit for the society,otherwise it is worthless and dangerous
to the country’s development.
Na kuongelea Vyuo
vikuu, sio tu
kunarahisisha uongeaji,bali ni rahisi hata kufanyia majaribio mapendekezo
yatakayotolewa huku tukitaraji matokeo kuligusa haraka sana taifa! Wanafunzi wa
vyuo vikuu wanatarajiwa kukamata nyadhifa au nafasi fulani sehemu mbalimbali za
kiutendaji, AMA
KUJIAJILI KAMA AMBAVYO HALI INAONEKNA KWA SASA, SAAFI SERIKALI YETU!,
hivyo basi kweli
kabisa wakikosa elimu bora ni hatari kubwa pengine kuliko hata kama wasingesoma.
Maana
ni bora kuwa na mtu usiyemuamini (Utakuwa makini) kuliko kuwa na unayemuamini
kumbe hastahili kuaminiwa! Na kibaya zaidi ni pale inapotokea anaongeza ufanisi
kuelekea kwenye kukudhuru. Yaani; Mfikirie Msomi ‘mbovu’ anapoamua kutumia
elimu yake kwa ajili ya kukutapeli, si ni afadhali asingesoma?
Is The Government aware of this poor quality of education?
Yes Of course.WENYEWE WANAJUA? NDIO?
Katika ripoti ya (President’s Office, Planning and Commission (POPC) (October
2012)), mtandao wa taifa, imeelezwa waziwazi kuwa
hali yetu katika eneo la idadi ya rasilimali watu na hata ubora kwa ujumla si
ya kuridhisha! Hivyo Serikali ina mikakati madhubuti ya kuboresha elimu ili
walau tuweze kuendana na ushindani na uhitaji wa soko la utandawazi.
Baadhi ya changamoto zilizoguswa na ripoti hii ni
- Wanafunzi kutojiunga na masomo ya sayansi;
- Matumizi kidogo ya teknolojia ya mawasiliano ICT
- Kutojitosheleza kiubunifu, ushindani na kadhalika katika utendaji wa kila siku!
Upambani wa hayo umeonekana unaweza kuwa kupitia:
- Vyuo maalumu na shule maalumu kwe ajili ya sayansi na technolojia
- Kuweka mpango madhubuti wa ushirikiano wa sekta binafsi na umma kwenye uendeshaji wa shule na vyuo hivyo maalumu
- Na pia kujidhatiti kwenye soko huria la pamoja la Afrika Mashariki
- Kuongeza idadi wanafunzi kujiunga vyuoni
- Kuboresha mazingira ya ufundishaji na kuwabakisha walimu katika kila ngazi
- N.k
MPAKA HAPO UBISHI HAKUNA, TATIZO LIPO, NA
TAIFA LINAJUA NA LINATUHITAJI TUCHANGIE MAWAZO JINSI YA KULITOKOMEZA TATIZO
HILI,TUTOE MAONI SIO KESHO TUNALAUMU KUWA WADAU HATUKUSHIRIKISHWA. KAMA KWENYE KATIBA,
KAZI YETU KUONGEA NA VYOMBO VYA HABARI TU! CHANGIA MAONI YAKO YA KATIBA SEHEMU
HUSIKA,HASA WALE AMBAO KWA MUDA WAO MWINGI WAKO NJE YA NCHI,LAKINI NDUGU ZAO
TUPO NCHINI NA PENGINE WATARUDI SIKU MOJA,TUPATIENI MAONI KULINGANA NA UHALISIA
WA HUKO,MSITUACHE TUDANGANYWE NA WANAO KUJA KUWASALIMU SIKU MBILI TU!
So, the need for the qualitative
effort in Tanzania Education is as urgent as it is.Tunaipongeza Serikali kwa kuliona hilo! Ila Tanki lina mchango kidogo katika
hili.
“Kikwazo
cha Maendeleo ya Tanzania kwa sasa
SI
IDADI YA WASOMI
BALI
NI
KUTUPWA KWA UBORA WA ELIMU”.
Elimu kuwa bora ni lazima iwe na zao la uzalendo ndani
yake!Bila hivyo ni ngumu elimu hiyo kulinufaisha taifa husika! Hata ukiangalia maana ya elimu kwa mujibu wetu wenyewe, na
ukafananisha na tunayo yafanya si tu makazini,hata katika familia zetu,unaweza
kuona ni WANGAPI AMBAO TUNA
BORA ELIMU NA WANGAPI TUNA ELIMU BORA. HIYO
HIYO ULIYONAYO,NI BORA KWELI?
Ukitumia
mfano wa Mwalimu Nyerere (Baba Wa
Taifa), kuwa wote mnaweza kula
rushwa,lakini mmoja kazi ikafikia ubora na mwingine hata isionekane.Mwalimu
alituagiza kuwa rushwa zote tuzichukie kama ukoma, japo sisi huchukia zaidi
pale ambapo kazi haikuonekana. Nafikiri ni vema basi tuchukie kazi
kutoonekana na tuchukie zaidi kazi kuonekana lakini bila kufikia kiwango, maana
sio tu kumetupotezea rasilimali,kodi zetu,muda, bali pia ni hatari kwa maisha kutumia kitu kibovu! Na
mara nyingi watu wanaotupatia Vitu vibovu huzaliwa na BORA ELIMU,ambayo huwa
haina KUHESHIMU MIIKO WALA UZALENDO ndani yake! Na inakuwa na upandikizi wa
MTAZAMO wa UBINAFSI saana!
WE BISHA LAKINI HATA ALIYEFUNDISHWA KUPIKA AKIPUUZIA
MIIKO,KELELE TU MEZANI! SIO MEZA HIYO! AHSANTE BA RIZI !
AU
“Kuna kitu kinaitwa mali ya UMMA. Kila mtu kichwani anamini kula ni
sawa ila mbaya kukutwa! Ni kwa sababu mtu kaambiwa kuna mali ya UMMA bila hata
kumjua UMMA ndiye nani HASA,basi hata kitu cha UMMA kinapoharibiwa mpaka
akatafutwe UMMA aje azuie uharibifu huo,hata kama mamia ya waTz tunaona,elimu
tuliyonayo haikutuambia UMMA NDIO SISI, haikutupatia fikra zenye UZALENDO na
zenye kuheshimu MIIKO ndani yake!”
BORA ELIMU HAITUFAI KABISA, TUPAMBANE NAYO
ZAIDI YA TUNAVYOPAMBANA NA UKIMWI
NA
‘Kama
elimu huikusaidii wewe na jamii yako kwanza ,maana yake ubora wake una mushikeri!’
Ubora kwa zama hizi, ni kama upendo,si kitu cha kusema utakigusa au pengine kukiona tu bali
inatakiwa ukihisi kutoka rohoni! Hebu mfikirie fundi nguo
anayekupatia nguo yako nzuri ya kuvaa harusini, baada ya siku yako ya harusi!
Unafikiri ni fundi bora,hata kama nguo hiyo imefikia kiwango ulichokitarajia?
Hata akikuambia amekusamehe malipo, bado hisia yako haitakuwa nzuri! Nyakati
hizi huyo sio fundi bora. ‘UBORA WA
KUNG’AA NA UDHAHABU UWEMO’,usitafute kwenye kamusi nimetohoa SI KILA KING’AACHO
NI DHAHABU,na msemo huu hautoki kwenye mtihani.
Kukosoa mikakati iliyowekwa na serikali utakuwa uongo,yaani ni “Ubongo Man”, kama Sharo
alivyotuambia, Mungu aweke roho
ya marehemu pema peponi! Ila kuchangia tu nafikiri ni muhimu na haswa
ndio ushiriki wenyewe!
Shule na Vyuo maalumu
nafikiri vitatusaidia, na pengine isiwe tu kwa ajili sayansi na teknolojia,
bali iwe maeneo yote japo hata kwa baadae!Hawa Wanasayansi
kwanza kwa sasa hawafui dafu kabisa kwa wanasiasa , sasa ni visuri tuboreshe na
Siasa/Uongozi kwa ujumla au huko mambo safi?
Tutake tusitake utofauti upo,hivyo wenye vipaji vya
madarasani wapewe nafasi yao kuvionyesha kama wale wa viwanjani na kumbini! Ukweli ni kwamba, tunapaswa kulinda
na kuheshimu akili zetu kama tunavyolinda migodi ya Geita na kwengineko!
Kwa sababu hata migodi inahitaji akili na fikra za watu
kwanza ili kutunufaisha! Tulianzisha Shule maalumu! Tujiulize Ziko Wapi?
Zinaishia Wapi? Kwa nini? Matunda yake yako Wapi? Hatuwezi kutegemea kufanya mambo makubwa kwa juhudi
ndogo? Kula bila Jasho mara nyingi kuna madhara makubwa kuliko faida!
Vyuo na Shule
maalumu, vinaweza kujenga ushindani, na kuibua utamaduni wa ubora bila hata
kutumia pesa nyingi. Nafikiri waliopitia shule hizo maalumu,hasa kati ya mwaka
1993 mpaka 2003 wanaweza kutoa ushuhuda wa hili.
Na itakuwa rahisi kwa serikali kuona ifanye nini na kundi hilo dogo na maalumu
kwa manufaa ya wengi! Upendeleo kama una maanisha manufaa ya wengi ni mzuri tu!Usiwanyime wanao wote kusoma,kisa
anayeelewa sana darasani ni mdogo na mkubwa,atajisikia vibaya! Mpeleke mkubwa
kwenye anachoweza zaidi,nani kasema kipaji cha uwezo darasani ndio bora kuliko
vingine! Mbona Kuna walichukia darasa kwa sababu ya kuulizwa kila
swali wao na wakafanya vizuria maishani kuliko waliofanya presentation mpaka za
tafiti za kitaifa?
Hatuwezi
kuwa sawa, hivyo hatuna haja ya kuukwepa utofauti wetu ,bali tuubariki na
kuuboresha,ili utuboreshee maisha badala ya kutuharibia.Ila
MUENDELEZO NI MUHIMU SANA,SIO UMAALUMU MWISHO A’LEVEL/DIPLOMA
TU! SIO SAWA HIYO.
Changamoto
nyingine zilizoorodheshwa zinaweza kujibiwa na nguvu ya soko, kama vile,kwa nini matumizi ya Ngamizi yako chini!Waafunzi hawajiungi na
masomo ya sayansi kulinganisha na wanavyojiunga fani zingine. Ubunifu na
ushindani katika ajira. Yote haya yanauhusiona wa moja kwa moja na kama soko la
ajira na utendaji wa kila siku unahitaji hayo mambo kiasi cha kumlazimu mtu
kuyatafuta au hata kupigia kelele kuwa apatiwe?
Nchi
jirani Ngamizi na Simu za mikononi pengine ni bei rahisi kuliko
Tz, kwa sababu zinasaidia
sana kwenye masomo,sisi tunahitaji zaidi
kitakachotusaidia kwenye FB,TWT na vingine kama hivyo!Hivyo hata ukiondoa ushuru wa
kuingizia Kompyuta (neno rahisi kuliko Ngamizi,kweli vya wenzetu vizuri
jamani) bei ishuke, sijui
kama tutanunua zaidi kuliko simu,ambayo full time
kuchart na ‘mafacebook gal/boi/mumy/dady/bro/sis/cou…..’!
Juu
ya Soko Huria La Afrika Mashariki! NO COMMENTS TODAY! Walimu waongezwe na idadi
ya wanafunzi vyuoni iongezeke,HIYO 100 MZEE, ila vyote hivyo ni hatarishi kwenye ubora
hivyo ni lazima viambatane na mfumo sahihi, kwa sababu HAVIKWEPEKI.
Na ieleweke kuwa Wanafunzi Tz na labda
duniani kote kwa sasa sio tu kuwa hatutaki kujiunga na masomo ya sayansi, bali
hata tuliosoma sayansi tunakimbilia Siasa na Biashara. Uliza SOKO LA AJIRA NA UJIRA, utapata jibu
zuri tu huhitaji kundi kubwa kutafiti kwenye mataasisi.
Tena
afadhali Serikali ilivyoleta mpango wa kupata mkopo ukiingia sayansi,sasa
nitafanyaje?HATA HIVYO, jamaa shahada ya kwanza anapiga mambo ya Kilimo,(Mkopo)
anaona kumbe dili ni kufanya kazi kwenye taasisi za kibiashara, anakopa
mwenyewe sasa, anasoma shahada ya pili biashara/sijua CPA na akimaliza tu
anagundua kumbe mambo yatakuwa rahisi kwenye kampuni yake akiwa ndani ya
siasa,hivyo anajiandaa kwenda Ph D / shahada ya Uzamivu sijui kwenye eneo hilo. Unafikiri nani anapenda
kuona anaumia sana halafu analipwa kidogo, na umri wa kufa unazidi kushuka?
NGUVU YA SOKO IMESHIKA HATAMU, uelewe
mitaa, la sivyo utakuwa unaona wenzio wanapita we hujui pa kuanzia wala pa
kutokea,SIJUI alimaanisha hivyo,
FID Q. Nguvu ya Soko inaongoza rasilimali
zipi, wapi na jinsi gani zigawanywe. Kijana mwenye AAA katika PCB na PCM
anashauriwa na mzee wake (Pro wa Hesabu/Dakt) kuwa mwanangu soma Masomo ya
Uhasibu/Sheria usije ukawa kama mimi! Huu ni WITO! Swali ni Nani akasome Hizo
Hesabu na Upasuaji? Mwenye AAA ya KLF?
Ni yaleyale tu ila
kwa mtindo ungine, zamani wazee walichezea madini bao wageni wakaja wakawapatia
gorori wakachukua madini, sasa pia tunachezea akili kali tulizopewa badala ya kuzalishia na wageni
watakuja,watatuletea makopo ya Kompyuta na TV halafu wanandoka na akili kwenda kuzalishia kwao! ASUBUHI
MPAKA JIONI TUNAHANGAIKIA JINSI GANI TUTAWAINGIZIA PESA WAO TU Wakati umefika Serikali ithamini Akili Kali na kuzitunza na kuzitumia kwa manufaa ya UMMA japo za
wachache! Kama huoni umuhimu wa akili, Jiulize; mimi ningekuwa raisi wa kwanza
TZ ingekuwaje leo? Sio mimi Wewe?
SULUHISHO LA HILI
Tiba ya haya ni pamoja na Kubadili
Mtazamo juu ya Elimu, Tuufanye ubora kuwa utamaduni wetu kuanzia majumbani, mashuleni mpaka vyuo vikuu! Ni vipi? Tutumie mfumo wa
menejimenti kwa kuangalia ubora utokanao na ujumla wa ushiriki wa wahusika (Total
Quality Management). Katika
mfumo huu, mteja anapewa nafasi kwanza ya kuamua juu ya ubora
unaopatikana, na nafasi ya pili kuwa kila muhusika ana jukumu
la kusaidia kuupata ubora huo,bila hivyo ni ngumu kuufikia huo ubora na tatu
ni kuwa katika utendaji, kila mtu ni mteja wa mwenzie,na kila mtu ana jukumu la
kuhakikisha mteja wake anaridhika kabisa na anachokipata.
Mfumo
si mgeni duniani, umeanzia kwenye viwanda huko Jepu,umesaidia hadi Yuesiei
tokea mpaka kwenye ujenzi, na sasa sekta za elimu zinanufaika pia!
Mfikirie mwalimu wa darasa la kwanza
anapowafundisha watoto kama wateja wake na huku akimchulia mwalimu wa darasa la
pili kama mteja wake wa ndani wa pili. Kwa kuhakikisha mwalimu wa darasa la
pili asipate shida hata kidogo atakapowachukua wanafunzi hao mwakani,na wengine
vivyo hivyo, vipi matokeo ya la saba! WATOTO WENYE ELIMU BORA YA MSINGI na SIO BORA ELIMU YA MSINGI.Na
kikubwa kabisa swala hili ni endelevu kwa kuwa mfumo huu unaamini kuwa siku
zote kuna mahali panahitaji uboreshaji hata uwe katika mafanikio kiasi
gani,ndio maana leo hii hata maanchi makubwa bado yanatafiti nap engine ndio
maana sio ajubu kuona matajiri wanaendelea kupunguza muda wa kulala wakati
mafukara tunaongeza muda wa kupoteza.
Kwenye elimu,mteja mkuu ni jamii
nzima,
na wateja
kwa ndani ni mwanafunzi na mwalimu,kila mmoja ni mteja wa mwenzake! Na
hivyo zao la shule ni wanafunzi wanaomaliza,jamii ndio itatoamajibu
kama inaridhishwa na ubora au la! Hivyo mwanafunzi anayemaliza na kufaulu
vizuri huku ni mwizi wa kupindukia jamii itasema hatufai,ikimaanisha hana ubora
wa kuifaa jamii!
Marekebisho yatarudishwa mpaka chuoni. Wakati kwa ndani,kama
mwalimu atakuwa kila wakati anahakikisha mwanafunzi wake ni mteja kwake, maana
yake yeye hayupo kama mwanafunzi hayupo,na mwanafunzi vilevile.Faida za mfumo ni nyingi kuliko ugumu na hata kama itachukua
muda mrefu kidogo kutoa majibu,lakini UBORA UKIWA MBELE KILA KITU KINAWEZEKANA KAMA JEPU AU YUESIEI, “ UBONGO ”?
“NAJUA TAYARI
INAONEKANA NI NDOTO, HII NI KAMA MADIWANI KUHUSIKA KWENYE MIRADI MBALIMBALI YA JAMII! HATA KAMA KUNA
MATATIZO KIDOGO BADO NI BORA KULIKO KUTOHUSISHWA, MAPUNGUFU YANAREKEBISHIKA,WALE
NI WATEJA WA MWISHO HIVYO WANASHIRIKISHWA ILI KUONA KAMA UBORA NDIO
WANAOUHITAJI?SAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAFI”.
“HEBU TUSAIDIANE, NI NCHI
GANI ILE WALIBAHATIKA KUPATA MAENDELEO?”
ZAID JUU YA TQM IN
EDUCATION: (Mpangule, J.A. (2009). Total Quality Management
application at Ardhi University. Dar Es Salaam: Unpublished Postgraduate
Dissertation Report at ARU.
ASANTE
MDAU KWA KUWA MMOJA KATI YA EFU MOJA WATAKAOFIKA HAPA CHINI! LAKINI UMESOMA
UMESCROLL?
Kama mdau, Maoni yako nini Juu ya hili!
0 comments:
Post a Comment