Kuna siku ambazo matokeo ya mchezo yanaeleza kila kitu.
Na kuna siku ambazo matokeo yanaeleza karibu hakuna kitu.
Mchezo wa kirafiki wa marudiano kati ya Mpaju FC Queens (ATINISU) na Prisons FC Queens ulikuwa moja ya siku hizo.
Own Thinking Tank
Hawa ndo vijana walio tung'arisha na bado wanahamu ya kufanya zaidi ya hapa...
Hiki ndicho kikosi cha Mpaju SC upande wa watoto kikiwa kwenye ziara katika shule ya msingi Mpolo.
Mpaju FC wakiwa kwenye Picha ya Pamoja wakati wa Tamasha la Mpaju Week 2019 Uwanja vya Magereza Mbeya.
Kuna siku ambazo matokeo ya mchezo yanaeleza kila kitu.
Na kuna siku ambazo matokeo yanaeleza karibu hakuna kitu.
Mchezo wa kirafiki wa marudiano kati ya Mpaju FC Queens (ATINISU) na Prisons FC Queens ulikuwa moja ya siku hizo.
![]() |
Picha ya pamoja ya Mpaju FC Queens kabla ya mchezo dhidi ya Prisons FC Queens.
Kwa mtu aliyeangalia matokeo pekee, angeona Prisons FC Queens imeibuka na ushindi wa mabao 3–0 dhidi ya Mpaju FC Queens. Hata hivyo, kwa wale waliofuatilia mchezo kwa karibu, walielewa kuwa mechi hiyo ilikuwa na maana kubwa zaidi ya matokeo.
PONGEZI NI MUHIMU NA MAFUNZO NI MUHIMU ZAIDI
Tunawapongeza TDS Girls kwa ubingwa wa WRCL 2025, ushindi unaoonesha maandalizi, nidhamu, na ubora wa soka la wanawake. Mafanikio yao ni kielelezo cha kile kinachowezekana panapokuwepo msaada na mipango thabiti. Ni wazi jitihada zinazofanywa kwao zitaendelea kusambaa Tanzania kote.
![]() |
| MPAJU FC QUEENS a.k.a ATINISU. "HATUCHOKI HATA TUKICHOKA" |
Safari ya Mpaju FC Queens (Atinisu) katika WRCL 2025, IMEISHIA NUSU FAIANLI, lakini imekuwa ushuhuda wa ujasiri, nidhamu, na kujitoa kupita matokeo ya kawaida ya soka. Licha ya changamoto kubwa za kifedha, uchovu wa safari, na upungufu wa wachezaji, wasichana hawa wamepigana kwa heshima na kulibeba jina la Mkoa wa Mbeya kwa fahari.