Saturday, March 13, 2021

LIGI YA MPIRA WA MIGUU KWA WANAWAKE - MKOA WA MBEYA

 MPAJU ATINISU WATISHA SANA

WAWACHABANGA TUKUYU QUEENS

NA KUSHIKA NAFASI YA TATU

Siku ya Jumapili ya tarehe 07 Machi 2021, historia iliendelea kuandikwa kwa Mkoa wa Mbeya na kituo cha michezo cha Mpaju Sports Centre. Haikuwa siku ya kuhitimisha Ligi ya Mpira wa Miguu ya wanawake hapa Mbeya, bali ilikuwa siku ya furaha sana kwa vijana wa MPAJU ATINISU yaani wasichana na wanawake wapambanaji wa Mpaju FC baada ya kupambana sana na kuhakikisha wanaondoka na ushindi mnono wa goli 2-0 dhidi ya timu ngumu na yenye uzoefu ya Tukuyu Queens

kutoka Wilaya ya Rungwe. magoli muhimu ya Mpaju FC Atinisu yalipachikwa na Jack ambaye aliwatoroka mabeki wa tukuyu kiustadi na kwa mbio kali na kuachia shuti lilimuacha mlinda lango akishangaa tu. La pili lilifungwa na Merry ambaye wengi walimwita MORRISON wakimaanisha amefanya mengi kwenye mashindano haya kama ambavyo mchezaji wa simba Sports Club (Luis Miquissone) alivyofanya michezo ya klabu bingwa Afrika. Picha zinaelezea mengi

KIKOSI CHA MPAJU ATINISU KILICHOLETA USHINDI NA KUSHIKA NAFASI YA TATU 

KEPTENI MARIA NA WACHEZAJI WA MPAJU ATINSU WAKIWA NA BAADHI YA WACHEZAJI WA MPAJU U-17 KATIKA PICHA BAADA YA USHINDI

MPAJU ATINISU WAKISUBIRI ZAWADI

KOCHA ALI MKUMBUKWA NA WACHEZAJI WA NA BAADHI YA MPAJU ATINSU 
 KATIKA PICHA BAADA YA USHINDI

VIONGOZI  MKOA NA MGENI RASMI KATIKA UTARATIBU WA KUFUNGA MASHINDANO

VIONGOZI  WAKITOA ZAWADI WA TIMU NA WACHEZAJI MBALIMBALI
MGENI RASMI (MKURUGENZI WA TIMU KEN-GOLD YA CHUNYA) AKIMKABIDHI KEPTENI WA MPAJU ATINISU MARIA STEVEN KAKWALE KITITA CHA PESA KAMA ZAWADI YA KUWA USHINDI WA TATU



MPAJU ATINISU WAKISHANGILIA ZAWADI




0 comments:

Post a Comment