Saturday, March 13, 2021

LIGI YA MPIRA WA MIGUU KWA WANAWAKE - MKOA WA MBEYA

 MPAJU ATINISU WATISHA SANA

WAWACHABANGA TUKUYU QUEENS

NA KUSHIKA NAFASI YA TATU

Siku ya Jumapili ya tarehe 07 Machi 2021, historia iliendelea kuandikwa kwa Mkoa wa Mbeya na kituo cha michezo cha Mpaju Sports Centre. Haikuwa siku ya kuhitimisha Ligi ya Mpira wa Miguu ya wanawake hapa Mbeya, bali ilikuwa siku ya furaha sana kwa vijana wa MPAJU ATINISU yaani wasichana na wanawake wapambanaji wa Mpaju FC baada ya kupambana sana na kuhakikisha wanaondoka na ushindi mnono wa goli 2-0 dhidi ya timu ngumu na yenye uzoefu ya Tukuyu Queens

kutoka Wilaya ya Rungwe. magoli muhimu ya Mpaju FC Atinisu yalipachikwa na Jack ambaye aliwatoroka mabeki wa tukuyu kiustadi na kwa mbio kali na kuachia shuti lilimuacha mlinda lango akishangaa tu. La pili lilifungwa na Merry ambaye wengi walimwita MORRISON wakimaanisha amefanya mengi kwenye mashindano haya kama ambavyo mchezaji wa simba Sports Club (Luis Miquissone) alivyofanya michezo ya klabu bingwa Afrika. Picha zinaelezea mengi

KIKOSI CHA MPAJU ATINISU KILICHOLETA USHINDI NA KUSHIKA NAFASI YA TATU 

KEPTENI MARIA NA WACHEZAJI WA MPAJU ATINSU WAKIWA NA BAADHI YA WACHEZAJI WA MPAJU U-17 KATIKA PICHA BAADA YA USHINDI

MPAJU ATINISU WAKISUBIRI ZAWADI

KOCHA ALI MKUMBUKWA NA WACHEZAJI WA NA BAADHI YA MPAJU ATINSU 
 KATIKA PICHA BAADA YA USHINDI

VIONGOZI  MKOA NA MGENI RASMI KATIKA UTARATIBU WA KUFUNGA MASHINDANO

VIONGOZI  WAKITOA ZAWADI WA TIMU NA WACHEZAJI MBALIMBALI
MGENI RASMI (MKURUGENZI WA TIMU KEN-GOLD YA CHUNYA) AKIMKABIDHI KEPTENI WA MPAJU ATINISU MARIA STEVEN KAKWALE KITITA CHA PESA KAMA ZAWADI YA KUWA USHINDI WA TATU



MPAJU ATINISU WAKISHANGILIA ZAWADI




Related Posts:

  •  MPAJU WEEK 2020(Disemba 15-22)Uwanja wa Magereza Chuo-Ruanda Mbeyanani kufungua Dimba timu za wasichana?MPAJU FCVS SUPER EAGLES Mpaju FCSUPER EAGLE… Read More
  • Udhibiti wa Idadi ya Wachezaji wa Kigeni Ligi Kuu Tanzania Bara Maamuzi ni vema Yakazingatia vizuri WAKATI WETU. Kama nimeelewa hoja, ni kuwa kwa kuwapunguza wachezaji wa kigeni walau kwa asilimia walau 50, kuna uwezekano tukaongeza nafasi ya wachezaji wa nyumbani kupata nafasi katika ti… Read More
  • WADAU WA SOKA JIJINI MBEYA WAFURAHIA MPAJU WEEK 2019 Washuhudia Mambo Mengi: Vipaji vikali, Uongozi Madhubuti wa Mpira Mbeya Mjini,  Ushirikiano wa wadau wa Mpaju SC na bila kusahau, Timu ya wasichana ya shule ya msingi ya Mpolo-Mbalali, Uso kwa Uso na Mdau mkubwa w… Read More
  •  MPAJU WEEK 2020“JAMII YETU-KIOO CHETU” Kauli mbiu ya Mpaju Week 2020 ni JAMII YETU NDIO KIOO CHETU. Mpaju SC inaamini changamoto zinazoizunguka jamii yetu zinatokana na kushindwa KWETU kuzitatua. Mpaju SC inaikifikishi… Read More
  • Ziara ya Mpaju SC Shule ya Msingi Mpolo 2020 haitasahaulikaKwa mara nyingine, Siku ya Jumamosi tarehe 29 Agosti 2020, Mpaju SC walitembelea shule ya Msingi Mpolo iliyopo Mbalali na kufanya michezo kadhaa ya kirafiki. Hii shule yenye hazina kubwa sana ya Michezo ya nchi hii. Mpaju ime… Read More

0 comments:

Post a Comment