Wednesday, April 2, 2014

Mnyonge nyi mnyongeni,Na Haki yake Mpeni



1
Tumlaani shetani, Ubinafsi Shetani.
Hana mpango shambani, Maisha yake angani.
Akishuka aridhini, Atashinda tu majini

Maumivu kijijini,Mijini yahusu nini.
Swali la kutoka lini, Tajiri ajibu nini.
Tajiri afanye nini, Kitufae masikini.
Mnyonge tumnyongeni,La Hakiye tumpeni
2
Mkulima masikini, Uchumi wako ni nini?
Kushinda kwako shambani, Faida yake ni nini?
Jasho lako la shambani, Hasa laliwa na nani?
Maisha kwako ni nini, Useme u kivulini?
Unajipinda shambani, Wanakupunja sokoni.
Kilimo kwanza ni nini, Maumivu kilimoni?
Mnyonge tumnyongeni,La Hakiye tumpeni
3
Jadala kuu bungeni, Si kilimo ni madini.
Pembejeo si shambani, Zinaliwa tu mijini.
Ujanja sasa nchini,Siasani si shambani.
Mababu wawe shambani, Vijana jaa mijini.
Somo kilimo shuleni, Wanafunzi huwaoni.
Misaada kilimoni,Yaishia tafitini.
Mnyonge tumnyongeni,La Hakiye tumpeni
4

Wakulima vijijini, Hebu jamani semeni.
Mafao yao shambani, Mipango yafanya mboni.
Kodi zote ni shambani, Hadi simu mikononi.
Kuenda uraisini,Kura upate shambani.
Chakula kote nchini, Kinatoka Vijijini.
Wengi wetu wa mijini, Hasa kwetu vijijini.
Mnyonge tumnyongeni,La Hakiye tumpeni
5
Shambani ni vijijini, Mijini pia shambani
Ni wapi leo mjini, Hapakuwa kijijini?
Ufukara mashambani, Umasikini mijini
Waziri awe shambani, Ubunge si luningani.
Reli kufika shambani, Nchi iko duniani.
Waziri daladalani, Mboni yetu ya mijini.
Mnyonge tumnyongeni,La Hakiye tumpeni
6
Kilimo kikumbukeni, Mnyonge msitirini.
Jasho lao masikini, Wabungeni lioneni.
Wasomi wetu vyuoni, Mkulima mjueni.
Wataalamu nchini, Faida yenu ni nini?
Sayansi yetu jamani, Itufaacho ni nini?
Tuache ulimbukeni, Tujali kwetu nyumbani.
Mnyonge tumnyongeni,La Hakiye tumpeni

7


Elimu ziko mijini, Shambani abaki nani.
Shamba si usanii, Mkulima ale nini?
Wajanja si vijijini, Nakana huo Utani.
Wajinga wengi mijini, Tukibisha tubisheni.
Loliondo kumbukeni, Babu naye wa mjini?
Tamaduni tuthamini, Taaluma   zi shambani.
Mnyonge tumnyongeni,La Hakiye tumpeni





Related Posts:

  • KHERI YA SIKUKUU YA EID EL FITRIKatika kuhitimisha mfungo Mpaju Sports Centre iliandaa futari ya pamoja kama inavyoonekana katika picha. Mbali na tukio hili kulenga kuhitimisha mfungo, pia ilitumika kama nafasi ya kuwaaga wachezaji watatu ambao wamechaguliw… Read More
  • KWA HERI ANITA BOUS,WEWE MBELE SISI NYUMA HAKUNA NAMNA NYEPESI YA  KUMUELEZEA "MJERUMANI" ANITA BOUS.  TUNACHOJUA ALITUPATIA UPENDO, UPENDO NA UPENDO. UONGOZI WA MPAJU FC UMEPOKEA KWA MASIKITIKO SANA KIFO CHA MMOJA WA WADUA WAO-ANITA BOUS (COLOGNE-GE… Read More
  • Mpaju Sports Centre Day- 31st Disemba 2019 Usiseme “MPAJU DAY”, Sema “MPAJU WEEK 2019, HATUA NI HATUA” Kauli mbiu ya Mpaju SC, ni BURUHANI INA MAMLAKA. Ikiwa na maana rahisi tu ya kuamini, kuwa binadamu, na hasa watoto wadogo na vijana wa kitanzania, wanayo… Read More
  • Safari ya Mpaju FC- Mbalali (Meta- Shule ya Msingi Mpolo)Kama ilivyo kawaida ya Mpaju Sports Centre,mwaka huu pia walifanya ziara ya Mechi za kirafiki katika Kijiji cha Meta,Mbalali Mbeya ili kucheza michezo kadhaa ya kirafiki na timu za Shule ya Mpolo waliokuwa wenyeji wao na Timu… Read More
  • Mpaju FC yaanza Kuitikisa TanzaniaMpaju FC imetoa dalili nzuri kwa mafanikio ya kituo cha michezo cha Mpaju baada ya vijana wake watatu kufanikiwa kuwakilisha kituo kwa kushiriki mashindano ya kusaka vipaji ya TFF kupitia mkoa wa Mbeya. Vijana Emmanuel Mbwilo… Read More

0 comments:

Post a Comment