Sunday, September 15, 2013

Mbeya City Yadhihirisha kuwa Inastahili kuwa Ligi KUU



 Mechi baina ya MBEYA CITY ya jijini Mbeya na YANGA yenye makao yake jijini Dar Es Salaam, zimetoka uwanjani na kukubali kuambulia pointi moja kila moja baada matokeo halali ya 1-1. 


“Timu za Yanga na Mbeya City leo zimetoka sale ya goli 1-1 katika mchezo mkali na wa kusisimua uliofanyika katika uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Timu ya Mbeya City ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika ya 50, liliofungwa na Mogani..............................................

Timu ya Yanga ilisawazisha goli katika dakika ya 75 goli lililofungwa Kavumbagu kwa kifua na kumuacha golikipa wa Mbeya City akigalagala bila mafanikio ya kuokoa mpira uliokuwa ukienda wavuni polepole.......................................................................................................................

Timu ya Yanga ndiyo iliyokuwa ya kwanza kuingia uwanjani saa 9:15, timu hii iliingia kwa mbwembwe huku basi lililobeba wachezaji likipita upande walikokuwa mashabiki wa Mbeya City, shabiki asiyejulikana wa Mbeya City alililirushia chupa ya bia basi hilo na kuvunja kioo cha pembeni cha mlango wa dereva na kumjeruhi dereva wa basi hilo, hali iliyoleta mtafaruku mkubwa kwa viongozi wa timu ya Yanga.” http://basahama.blogspot.de/

Tanki, lina mawili matatu juu ya matukio yote ya mchezo kama ifuatavyo:

1.      Mtazamo wa mechi Kifikra

Washabiki wengi wanaonglea mchezo kuwa ulikuwa mkali, kitu ambacho ni kawaida sana kwa Tanzania. Japo, kwa kuyatazama matokeo, jambo hili linakribiana na ukweli sana. Yanga moja kati ya timu kongwe nchini, ikiwa ni pamoja na watani zao Simba (ambao wao wamefanikiwa kuwalaza Mtibwa 2-0), ina rasilimali nyingi sana (Ikiwa ni pamoja na kuwa Bingwa mtetezi) ukifananisha na Mbeya City. Hivyo, ukali wa mchezo huo kwa kiasi kikubwa unachangiwa na ukweli kuwa MBEYA CITY, wamekuwa wakijaribu kuthibitisha uwezo wao. Jambo hilo,bila shaka vijana hao wa Kocha maarufu Mwambusi, wamefanikiwa kuuonyesha, na hasa ukizingatia baadhi ya matokeo yao ya kuridhisha waliyopata siku za nyuma. Japo,kukataliwa kwa goli moja la Yanga kuna paswa kuwafanya MBEYA CITY, watambue hasa wapi walipo kisoka,na kutojisahau na kulewa sifa. 

Mambo mengine kadhaa yanayoweza kuambatana na matokeo haya, ni aidha Ligi ya Tanzania bado ni dhaifu, ndio maana vinara wa soka hawana uwezo wa kuzifunga timu ndogo, ama pia kinyume chake,yaani ligi sasa inaanza kuwa bora, kwa timu ndogo na ngeni kutoa ushindani sahihi kwa mabingwa watetezi. Lah pengine ubabaishaji wa mambo kama vile uzalendo na kupenda timu au rushwa za kijinga, umepelekea timu moja wapo kutotoka na ushindi.

Jambo kubwa, la kulitazama pia katika mechi hii ni swala zima la uzito wa timu hizi mbili. Mbeya City haijai kwenye KIGANJA cha Yanga. Lakini kuna washabiki kadhaa, wamefurahishwa na uwezo ulioneshwa na vijana wa MBEYA CITY. Hili linatufundishwa kuwa UWEZO UPO, sio mpaka tutafute wachezaji NCHI za watu, wakati mafanikio hatuyaoni, ZAIDI ya kuwapatia PESA nyingi sana. Tuthamini vyetu, ili VITUFAE jamani. Na Zaidi, ni kuwa hizi TIMU zetu kubwa zinazoonekana kama ndio msingi wa soka zinapaswa kujifunza hilo sana,zinaweza kutanua wigo wa miliki zao na kupta wachezaji toka mikoani. Na Zaidi TFF, kujifunza kuwa SOKA la BONGO, kwa ujumla haliishii JIJI la DAR, kuna umuhimu wa kuboresha MAONO yake na kuzikia timu za mikoani, badal ya kuzifanya wasindikizaji wa SIMBA NA YANGA.

2.      Mtazamo wa  TUKIO  Kifikra

Mechi imekuwa gumzo, na shamrashamra nyingi sana katika jiji la mbeya. Kuna mengi mazuri ya kufurahisha na mabaya ya kusikitisha yaliyojitokeza kama ambavyo picha zimeripotiwa na Basahama.kila mtu ananafisi ya kuyachambua haya kwa jinsi anavyoweza, lakini Tanki lina haya machache kwa Watnzania na Wana Mbeya, walio mashabiki na wasio mashabiki wa SOKA la BONGO.

·         UMUHIMU WA MICHEZO

Ni vema sasa wana MBEYA, tukaona umuhimu wa michezo, kuwa ni Zaidi ya ajira za ualimu ama kazi nyingine amabzo tumekuwa kila siku tukizipa kipa umbele, kwa sababu MPIRA humgusa kila mtu kuanzia mpiga debe mpaka muuza juice. Mabil na vijana wetu wenyewe na pengina faida mbalimbali za kiafya na kadhalika. HUU ni UCHIZI wa DUNIA, sasa TUCHIZIKE NAO. Timu zetu zipewe kipaumbele, na mipango madhubuti, iwekwe. Isije ikawa Mbeya City, kesho akiondoka Fulani,inaanza kusuasua, kama vile ilikuwa inamnufaisha yeye, wote tulishuhudia uwanja wa sokoine ulivyodolola siku kadhaa tulipokuwa hatuna timu katika LIGI KUU. Hata JIJI pia lililala kabisaaaaaa! Leo hii, watu kutoka Tunduma, Chunya na Tukuyu wanaungana uwanja wa SOKOINE, nafikiri wanauchumi wanaweza kutueleza ni kiasi gani mechi hiyo imeinufaisha MBEYA nzima, mbali na YANGA, MBEYA CITY na WALE AKINANIHII wanaotuzuilia maendeleo ya SOKA.

·         UWANJA WA SOKOINE

Jamani, tumeona jinsi gani UWANJA ulivyombovu, kuanzia kweny sehemu ya kuchezea, mpaka sehemu za kukaa. Hivi haya nayo tunasubiri AFUFUKE MWALIMU aje aseme WANAMBEYA rekebisheni uwanja wa SOKOINE. Hata kupigwa chupa kwa gari la Yanga ,ni kukosekana kwa usalama wa kisasa, ambapo wachezaji wanaingia uwanjani kwa usalama kabisa. Sisi si wendazawazimu wa soka kiasi hicho, ukilinganisha na nchi fulanifulani duniani. Ukiuliza utaambiwa, uwanja ni wa FULANI, hivyo, sijui kikaenda kikarudi,siasa tupu. Kama FULANI ndio mwenye uwanja,basi atambue ni kiasi gani, amekalia pesa, na ni kiasi gani analiumiza jiji na ni kiasi gani anawanyima wananchi wa Mbeya maendeleo ya kweli, lakini zaidi huu ni UZEMBE WETU  WANA MBEYA tu. Tunashindwa kukarabati uwanja, na hata IKIBIDI KUJENGA uwanja MPYA wa maana ukabadili na SURA ya jiji letu?

Chochote, kinachotuzuia WANAMBEYA kuwa na UWANJA bora wa SOKA, tukichukie kama UKOMA. PESA ZIPO, WATAALAMU wapo, na UWEZO UPO kabisa. Kinachokosekana ni FIKRA BORA TU, na NIA. Ubinafsi, umetujaa, hakuna anayeangalia watoto wetu kesho wanahitaji nini, tunakula mpaka kile tutakachokihitaji wakati wa uzee wetu! Kila kitu, tunaamini kinatakiwa kiwe DAR!

BAADHI YA PICHA ZA TUKIO ZIMA NI HIZI HAPA (CHANZO: BASAHAMA BLOG)

BASI LA YANGA
MASHABIKI WA MBEYA CITY


MASHABIKI WA YANGA

MASHABIKI WA YANGA WAKITOKEA TUNDUMA

WANA HABARI MBALIMBALI MBELE YA SEHEMU MAALUMU YA UWANJA

KIKOSI CHA MBEYA CITY DHIDI YA YANGA

GARI LA YANGA,SEHEMU ILIYOPIGWA TUPIWA CHUPA NA KUMJERUHI KIONGOZI MMOJA

VIKOSI VIKIKAGULIWA

MAKAPTENI WA TIMU WAKIPATA PICHA PAMOJA NA WAAMUZI

KIKOSI CHA YANGA DHIDI YA MBEYA CITY
 

0 comments:

Post a Comment