Sunday, November 10, 2013

Architectural Technology (ATy), Kibongobongo ni nini?



Kuongelea Taaluma usiyoijua na hasa kama hii, kidogo mtu unapaswa kuwa jasiri, ama chizi kabisa kama alivyoasa mwalimu Nyerere juu ya kugusa mambo ambayo wengi wamekwisha yafanyia kazi na kuamua tofauti na unavyodhani. Na watanzania ni wepesi wa kumchukia mtu anapoonekana kuwa muongo,Tanki linaomba watanzania wasilichukie kama huu pia ni uongo kwa sababu katika maisha, mara nyingi kuelewa ni kugumu kuliko kutafsiri, hivyo maana inaweza kueleweka kitaalamu na kikawaida na ama vinginevyo. Tanki, linawakilisha uelewo wa vinginevyo kama mbongo, na hivyo kutoa nafasi kwa wataalamu kutoa mwanga zaidi na sahihi katika mjadala huu muhimu kwa taifa letu. Architecture (A) ni Taaluma ya usanifu wa ujenzi, kimsingi kwa Tanzania
taaluma hii inahusishwa Zaidi na ujenzi wa nyumba japo inaweza kusaidia hata madaraja na ujenzi wa namna hiyo pia. Kueleza Maana kunahitaji ujasiri ambao tanki kwa leo halina. Lakini, tofauti na vile wengi tulivyozoea, kuwa Architects (As) wanachora ramani za nyumba tu, wataalamu hawa huwa wako mbali Zaidi ya hapo. Huwa wanatafsiri yale ambayo mtumiaji na mhitaji wa jengo anayawaza ama anatamani kulingana na taratibu zote za kisheria za ujenzi na mahitaji ya kitaalamu ya ujenzi, ikiwa ni pamoja na kulipa jengo hilo nakshi sahihi kumridhisha mtumiaji na mhitaji. Ni wasanii, wanasayansi na pengine ni wafanyabiashara vilevile. Naipenda maana iliyotolewa na mmoja waigizaji wa SERIES ya MISSING, kuwa (A) ni taaluma ya Hesabu,Uhandisi na mchanganyiko fikra za Kisanii.Labda alisahau tu kusema na yenye kuhitaji mtzamo wa kibiashara pia.
Baada ya muda mrefu, kumejitokeza taaluma nyingine karibia sawa kabisa na hii iitwayo Architect Technologist (ATs). Kimsingi tofauti ya hizi taaluma mbili inaanzia kwenye majina yenyewe. Yaani, Zaidi Architects (As), ATs wao wanapaswa kuubadili usanifu/ubunifu wa majenzi hayo yanayofanywa na As, na kuyafanya yaweze kujengeka kirahisi ama kiufanisi na kiteknoljia zaidi. Kimsingi tanki linawatazama wataalamu hawa, ATs kama wasaidizi wa karibu na washirika wa baadae wa As. Washirika wa karibu kwa sababu wameandaliwa kupokea na kubadili usanifu kwa ufasaha kuliko wasaidizi wa siku za nyuma, Architect Technicians (ATNs), ambao hawa ni wasaidizi wa wote. Na ni washirika wa baadae kwa sababu kwa namna moja au nyingine ATs wanaweza kuendesha miradi ya kiwango Fulani bila shaka na baada ya uzoefu Fulani, wanaweza kushiriki kwenye miradi kama wataalamu wenza wa As.Yaani, kufikiria jengo sahihi kwa kazi fulani (Hoteli)-As, na kuionyesha inavyofanya kazi vema Ngamizi/kompyuta (ATs) ni vitu viwili tufauti. Na zaidi kama unaweza kusema vigae hivi vitasaidia kuzuia joto  kiasi fulani lisipotee vyumbani, lazima uwe unajua vigae hivyo ni vya aina gani na vijengweje. Hivyo hivyo kwa rangi na kadhalika na hata mengine kama vile kusema UMBO HILI haliwezekani kujengekeka, wakati hakuna aliefanyia tafiti kuthibitsha hilo, zaidi ya yule anayesema haliwezekani.
Kama ilivyo ada kwa binadamu, ni WABISHI sana kukubali WAZO JIPYA. Kuna wataalamu waliuawa kwa sababu tu wanasema dunia sio bapa. Hivyo hivyo, kwetu Tanzania, mpaka sasa kuanzishwa kwa ATs kunaonekana kama ni kwa kisiasa Zaidi, maana mijadala juu ya kuwatambua wataalamu hawa inachukua muda mrefu na sura tofauti kiasi cha kuwafanya vijana wanaomaliza vyuo kama ATs, wajiulize kama walifanya chaguo sahihi au la! Ukithubutu kuongelea, utaulizwa maswali magumu mpaka ujute, lakini swali kubwa ni, je kutokuongea ni kwa faida ya nani? Wengi hawapendi kusikia maneno ya mitaani, hasa wataalamu na wanasayansi, lakini wanasiasa wengi wanafanya vizuri kwa kuanza kusikiliza maneno ya mitaani, maana FUNUNU ndio mwanzo wa tafiti. Kufuatia ujinga huu wa kijiweni, Tanki lina mawili matatu kwenye eneo hili.
 ARCHITECTS
Kwa ujumla hawa ndio wakuu wa taaluma hii nchini. Mabadiliko yanapaswa kuanzia kwao kama tunataka yatuletee manufaa kirahisi. Imekuwa kawaida kwa taaluma mbalimbali kama hizi kumegwa ili kuongeza SPECIALIZATION. Tumeona kwenye Wakadiriaji Majenzi,Wapimaji na ramani,Wahandisi Umeme,Mawasiliano na hata Ustawi wa jamii na Utawala. Kwa mtazamo huo, pengine ni wakati sasa kuwaruhusu wengine pia washiriki katika KEKI yetu. Hili lina faida wakati Fulani, ya KIFANISI na KIUCHMI kwa WOTE. Muhimu ni kujiuliza, ni kweli As wanahitaji ushiriki wa ATs, ama ni misukumo tu ya kisiasa inaingilia taaluma? Ama swali jepesi, ni kama kati ya Architect na Architect Technician tunahitaji mtaalamu mwingine kulingana na mahitaji ya Taaluma kiutendaji. Kwa mfano; TIMU ya ujenzi  ikiwa na  CLERK OF WORKS, mwenye taaluma ya ATs, inaweza kuongeza ufanisi Zaidi? Kweli kuna UPUNGUFU, kati ya USANIFU/UBUNIFU na UTENDAJI/UHALISIA, ambao TEKNOLOJIA inaweza KUZIBA pengo?
As wanapaswa kuwakaribisha kwa ROHO safi ATs KAMA, wanakuja kuboresha TAALUMA na kuifanya ikamilike kwa kuziba PENGO HILO. Na wana paswa KUONYESHA kwa vitendo kwa WATEJA wao, yaani WATANZANIA kuwa ATs wataleta madhara tu, maana WAO wanatosha na WANATEKELEZA sit tu yote bali na Zaidi ya ambayo ATs wanakuja kuyafanya. Hili ndio sahihi, kwa sababu litaonyesha kuwa ATs hawahitajiki, na pia kuna madhara kuwa nao. Lakini, ikiwa ni maneno tu, inakuwa na mushkeri. Pengine kuna upungufu umekuwa ukiwakera WATANZANIA, ila tu kwa sababu hawajui kama unawezekana kuondolewa, wakawa wanaendelea kuvumilia,na pengine hawajui radha nyingine. Maana wanasema motto akizoea chakula cha mama yake huamini ndio bora kuliko kingine.
ARCHITECTS TECHNOLOGISTS
Inaaminika kuwa NADHARIA bila VITENDO ni BUTU na VITENDO bila NADHARIA ni UPOFU. Hili linaweza kufanana kidogo na hizi taaluma. Msingi wa ATs ni kuweza kutafsiri taswira ya As na KUWEZA kuiunganisha na UHALISIA kwa watendaji wengine kiufanisi Zaidi kupitia TEKNOLOGIA. Hivyo kimsingi hawa sio wataalamu wa KUTAFSIRI TASWIRA ya TAJIRI, na kuifanya IUNGANISHWE na UNAKSI WA JENGO, SHERIA NA TARATIBU ZA UJENZI na MAHITAJI YA WATUMIAJI. Wanaofanya hili ni As. Kwa mtazamo huu, ATs wanapaswa kujikita kwenye eneo lao la KIUTENDAJI Zaidi. Kimsingi wanapaswa kujiandaa kuwa na ubunifu,utashi na uwezo katika uelekeo huo kwa kutumia Teknolojia sahihi. Kama mafunzo na maandalizi yao yatakuwa yakiishia kwenye uelekeo wa As na ATNs Zaidi, itakuwa UTATA. Mazingira yanaonyesha hali hii ya Utata ndio KIKWAZO,maana inakuwa kama TANZANIA inaongeza As wenye UPEO usioridhisha sana wa KISANIFU na kuwabandika NEMBO ya ATs, kisha kuwamwaga SOKONI ambako wanaenda kufanya kipande ama kazi yote ya As,yaani wanapewa nafasi ya kuonja keki kwene sherehe isiyowahusu wakati waalikwa bado wako kwenye foleni. Kikwetu hii huwa inauma sana,hata kama mwalikwa pia hakuchangia,anaweza hata kufoka na kuharibu sherehe kabisa.
Kwa hiyo ATs, wanapaswa KUWAONYESHA As nini hasa Tofauti yao na WAO kwanza. na ni nini hasa tofauti yao na ATNs. Na zaidi, Wanaoamini kuwa ATs ni muhimu na ATs wenyewe, wanapaswa kuwaonyesha WATANZANIA kwa Ujumla ambacho WANAKIKOSA kwa kutoka na As, ama WANACHOATHIRIKA kwa kuwa na As bila ATs. Bila kusahau pia, kuwaonyesha As na ATNs, wanachokikosa kwa kuwa pekee yao bila ATs.
UJIO WA BUILDING INFORMATION MODELLING-BIM
Hili ni zao la teknolojia, sasa dunia inakimbilia kwenye kuhakikisha kila mtu anashiriki kwenye mchakato wa ujenzi kwa uwazi kabisa kupitia HIFADHI ya pamoja ya taarifa zote za kitaalamu. Moja kati ya vikwazo vinavyojitokeza ni ugumu wa As katika  kushirirkiana na ATNs. Mawasiliano yamekuwa kikwazo katika kuongeza ufanisi na tija kwenye sekta ya UJENZI. Wakati BIM inaonekana kutatua hili, na kukubaliwa dunia, sisi tunajiuliza kama tuwakaribishe ATs au la.Kama BIM itashika moto nchini, ATs ni wataalamu ambao tutawahitaji sana kuhakikisha tunafanya vizuri. Hii ieleweke kuwa hapa ATs ni utaalamu na sio cheti cha usajiri au cha kuhitimu cha ATs.
BIM inawezesha TAJIRI/CLIENT kuhusika na kuona jinsi jengo litakavyoweza kuwekwa kwenye ardhi, katika uhalisia wake kabla ya kwenda kujengwa,ama jinsi mwanga wa asili utavyokuwa unapunguza matumizi ya umeme. Haya na mengine mengi yatahitaji sio tu muda bali mafunzo, ambayo pengine yakawa sio tu ATs bali hata watu wa ICT, ambao mara nyingi huchukuliwa kama ni watu wa baadae sana. Lisemwalo lipo, UMIMI unaondoka jamani, ni vema tukaondokana nao kabla haujaondoka na sisi.Kama ATs ni wataalamu muhimu katika kuharakisha BIM nchini, maana yake mjadala utanuke zaidi na kuona ni jinsi gani tunajichelewesha kukamata soko la afrika katika Ujenzi. Maana BIM mpaka sasa ni sehemu chache tu ambazo zimejaribu kutumia ikiwemo bondeni pale kwa mzee Madiba.
WASHIRIKA WENGINE WA UJENZI
Ujenzi una washirika wengine wengi kama wahandisi na wakadiriaji majenzi. Hawa wote wana vita zao za ndani kwa ndani, hata kama kwa namna moja au nyingine hazijafikia mahala pa kulipuka. Nao pia hawana budi kujiuliza kama UJIO wa ATs, ni neema ama hatari kwao? Kwa kawaida ujenzi unategemeana sana, na hivyo kama wengi wataona ujio wa taaluma hii ni neema, hawana budi kuwaambia WATANZANIA haraka kuwa ATs ni muhimu. Huu sio wakati wa Bodi ya wahandisi kujitenga na bodi ya Wasanifu na Wakadiriaji majenzi, ama kujitenga na bodi ya wakandarasi. Ni wakati wa kuunganisha nguvu na kudumisha mawasiliano na kuona ni wapi sekta ya ujenzi inaenda. Ni vipi sekta hii itaondokana na kuomba msaada wa KUPENDELEWA na SERIKALI na kuwa inaomba KUISAIDIA serikali. Ni wakati wa kuona washiriki wake wanaogopwa nje ya mipaka ya TZ, kwa uwezo na sio vinginevyo. Na ni wakati AMBAO ukweli ni kuwa KUKUMBATIA KAZI,TAALUMA, NA kadhalika ni KUJINUFAISHA kwa KUTEKETEZA TAIFA. UBORA wa sasa HAUPATIKANI bila ushiriki wa kila mtu ipasavyo.
MTAZAMO/MONI/PENDEKEZO/n.k
1.     Pengine hili sasa kwa NCHI kama TANZANIA linamaanisha kupokonya KEKI kubwa ya As, kwa sababu kwa Mtanzania habari ya UNAKSI na UTAALAMU sio MUHIMU labda kwa MIRADI mikubwa sana,ambayo pengine haichukui asilimia kubwa ya kazi za Wataalamu hawa. Lakini maslahi ya watanzania yanapaswa kupewa kipaumbele, kwa maana ya UBORESHWAJI wa TAALUMA na HUDUMA na SIO vinginevyo. Kama ATs hawafai, tufute, maana vijana wanazidi kumaliza, na kama tunamashaka na ubora, basi wasajiliwe (kwa muda chini ya As), wakati tunapembua Zaidi. Kuna umuhimu wa kujadili kitaifa Zaidi, ili tujue undani badala ya kulisikia chinichini, na pengine hata wafanya maamuzi wakiulizwa hawalijui kabisa. Ni kawaida sana mambo kuzuiliwa kwa hofu ya KIMASLAHI ZAIDI ya KITAALAMU. Na matokeo yake ni kudhorotesha maendeleo ya VYOTE kwa WOTE.
2.  Dunia haitusubiri sisi, TEKNOLOJIA inakimbia. Mfano mwepesi ni ujio wa Building Information Modelling. Ni wakati sasa tutambue kuwa Teknolojia ni kitu chenye uzito wa peke yake, na kama hatutakiheshimu, ni wazi kuwa tutatupwa nje ya SOKO. SIjui kama wakati Tanzania inaanza kutumia Ngamizi, Kompyuta, kufanya usanifu, kama kulikuwa na usumbufu wa namna hii au unaofanana na huu. Maana kama hali ilikuwa hivyo, basi huenda imechangia kutuchelewesha katika matumizi ya Ngamizi kwenye taaluma hii. Leo hii naamini As wanaotumia na wasiutumia Software mbalimbali, kama ARCH CAD,AUTO n.k kadhalika watakuwa wanashirikiana vizuri na wanajua maana na tofauti ya pande mbili, yaani teknolojia na sayansi ya taaluma katika utendaji. Kwa mtazamo huo huo, nafikiri tunaaswa kutambua kuwa ukijikita kwenye sayansi a taaluma una weza kukosa uwezo sahihi wa kiteknolojia, na hivyo kuhitaji mwingine kubobea kwenye eneo hili ambalo ni muhimu kwa maendeleo ya pamoja.
3.     Taaaluma kama hii ya (A) sio ya kuifanyia mzaha, na kuifanyia USOKO huria kama ambavyo tunafanya kwenye vitu vingine. Hii ina maanisha, ni lazima kuwe na tafiti sahihi, kuhakikisha kuwa uamuzi unaochukuliwa ni wenye kulinda UBORA wa taaluma na MAISHA a watu. Hivo hata ATs, wanapaswa kulijua hili, na kutochukulia kama wanazuiwa kwa maslahi binafsi, hata kama kutakuwa na ukweli. Kilicho sahihi ni kufikiria kuwa, vyovyote iwavyo wanazuiwa kwa SABABU kuu YA WATANZANIA, wakiwemo watoto na wajukuu wao mpaka vitukuu vyao. Na Zaidi ni wenyewe, maana tuendako, bila misingi imara, yeyote anaweza kudhulika wakiwemo wao. Lakini, pia kwa upande huo huo, tutambue pia kuwa MAZINGATIO ya ujenzi ya MWAKA 47 na sasa ni tofauti. Leo,mazingira,ubora,gharama n.k ni vitu vyenye sura tofauti na siku za nyuma. Hii ina maanisha, mtaalamu wa zamani aliweza kuzingatia vitu vichache na kwa uchache nab ado akakubalika, kuwa kafanya kazi timilifu. Lakini leo nguvu ya soko na utandawazi umeleta taswira tofauti juu ya utimilifu wa kazi, na hivyo, kama mtaalamu ataendelea kuwa na mzigo mkubwa, kuna uwezekano mkubwa sana, akatoa sio tu kazi timilifu bali hata kazi isiyo na ubora timilifu, kitu ambacho kinawiana kabisa na KUHATARISHA MAISHA ya watumiaji kwa KUWARUHUSU ATs kuvamia Taaluma. Tunajione maamuzi mengi ya kisiasa yanavyotudhulu kwa kumbukumbu za mwalimu alifanya hivi ama mbona tulikuwa tunafanya hivi tu na kitu kinajipa.
 Makundi na shindani sio mbaya, kwa sababu taaluma hizi zina asili hiyo. Yaani, watu hucheka na kuongea wkiwa nje ya kazi, lakini wanapoingia kaziani, ni ushindani na utaalamu tu vipaswa kupewa kipaumbele. Kinachojitokeza sasa ni upandikizi wa ushindani na chuki zisizo na tija, yaani kama akinananihii. Hili sio zuri, lakini kama waswahili wasemavyo, AKIMWAGA MBOGA, MWAGA UGALI, mkiumwa njaa mtaelewana.
Kama kawa, WABONGO, cha kwanza ataangalia REFERENCE ili aanze kubishana. Lengo hapa ni kuamsha hamasa ya kulielewa hili swala kwa undani, kujua kama kuna umuhimu wa kumwaga mboga,ili wote tusile.Swala la kasema nani, kwa sasa sio muhimu,muhimu ni MJADALA juu ya ATs  Tanzania, kama sehemu ya kuboresha ARCHITECTURE na UJENZI kwa ujumla. Na zaidi ni kuwa kuna umuhimu wa kujadili mambo katika mtazamo wa Kitaifa zaidi kuliko kimaslahi ya kitaaluma.
 SWALI LA KIZUSHI: Architectural Technology, tuna TAALUMA AU JINA?
…………IT IS JUST THE BEGINNING………………

2 comments:

  1. i like it sir...ni changamoto nyingi tumeshakutana nazo sana huku makazini kuna wanaojitahidi kuelewa na wengine kubeza kabisa...utata unakuja hapa sisi ni kina nani na kazi tunazofanya ni zao pia na ni kina nani wametu train .....wabezaji husema architects ndo walio tu train kwa hiyo tutabaki kuwa ATNs....napenda kukili makosa ya sisi tuliotangulia huku mitaani japo tunafanya kazi as kupata pesa kwa sasa ila HATUNA UMOJA kabisa juu ya hili...wakati tunasoma tulikuwa tunafikilia kumaliza na kuingia mtaani...hatuna mwongozo wala ukweli juu ya elimu hii. sasa INATUPASA KUWA NA UMOJA NA KUUNDA MOVEMENT za kujulisha uma sisi ni kina nani.....

    ReplyDelete
    Replies
    1. Uko sawa, kuwa na umoja ni muhimu. Ila mjue umoja wenu haupaswa kuwa na lengo la kubishana, bali kuwabainishia watumia huduma yenu tu,kuwa nyie sio wao na ni nini wanakosa kwa kutowatumia nyie. Na njia nyepesi ya kulifanya hilo, NI KUFANYA KAZI katika UBORA wenu, yaani wenye UTOFAUTI ni WAO.Naamini, HATA Architects, waliomakini wanajua ni jinsi gani wanahitaji ATs. Tatizo la TZ, huwa hatujui kwa nini tunahitaji kitu fulani, ndio maana mtu anadhani kuwa TECHNICIAN maana yake,kufanya kazi chini ya MTAALAMU kama MBUMBUMBU,kuwa HUNA LOLOTE MBELE YA MTAALAMU. Kumbe HAO NI WATU WAWILI TOFAUTI, wanaotegemeana katika utendaji .Dunia ya sasa hata TARISHI ANA UMUHIMU WAKE OFISINI, hivyo MAISHA ni ya kutegemeana zaidi ya KUENDESHANA. Muda si mrefu majibu mengi ya matatizo ya namna hii, yatapatikana. Nashukuru.

      Delete