Sunday, March 23, 2014

Uchama si ufitini, Ukabila si udini



1
Sasa mimi naamua,Maji nguo navulia.
Sifuri ukiijua, Utaandika na mia.
Bora kiguru na njia,Tuli bure huumia.

Kufika ukikawia, Pata ulichofikia.
Sikia ya kusikia,Maanaze dadavua.
Upande wako dandia,Undaniwe pambanua
Uchama si ufitini, Ukabila si udini
2
Kimbia ama tembea, Linganisho fikiria.
Matamu yao Ongea, Hakikisha wayajua.
Bweteka sio tulia, Hutakosha sufuria.
Kesha mvua na jua, Ya muumba fikiria.
Panga hata kwa jambia, Ya muhimu zingatia.
Mwenye kweli yenye nia, Nyendoze huwa sawia
Uchama si ufitini, Ukabila si udini
3
Yavuma kupindukia, Pasuka utasikia.
Katu usije kimbia, Tukioni sogelea.
Ngoma ikishatulia, Mizuka itapungua.
Kelele zitapungua, Hasara tutaijua.
Ujinga utapotea, Welevu tutaujua.
Umoja utajongea, Hesabu zitatukaa .
Uchama si ufitini, Ukabila si udini
4
Kushoto ama kulia, Hakuna kulotulia.
Zamani kushikilia, Ujinga ulotulia.
Ujinga kuurukia, Uchizi wa kudhania.
Dini kupuuzia, Sayansi kutoijua.
Kabila kuinamia, Gizani kutokomea.
Akili ukitumia, Ya moyo utapembua.
Uchama si ufitini, Ukabila si udini
5
Sifuri ukiijua, Muhimu utagundua.
Uchama wetu pembua, Viini vimeungua.
Udini wetu chungua, Uungu hutoujua.
Ukabila sio pua, Hatukosi kupumua.
Ukweli sasa gundua, Sifuri kutoijua.
Welevu wameng’amua, Wapi pa Kututungua.
Uchama si ufitini, Ukabila si udini
6
Napenda sana ongea, Machache ninayojua.
Kusoma bado kujua,Ubovu yangu tabia.
Sifuri yangu fichua, Fikira ziwe sawia.
Uchama ningechagua,Fitina wapi kwepea.
Kabila sito kimbia, Ukabila napembua.
Udini wangu wa poa, Mbinguni nime potea
Uchama si ufitini, Ukabila si udini
7
Fikiria dadavua, Kosoa nilokosea.
Sifuri yako chagua, Vema nami nikijua.
Tanzania yaungua, Huamini we funua.
Uchama wafurumia, Ujinga kushabikia.
Udini unachanua, Hakuna wa kuzuia.
Ukabila tunafufua, Ujinga umekolea.
Uchama si ufitini, Ukabila si udini





Related Posts:

  • NYERERE BABA WA TAIFA WA KUJIVUNIA ulius Nyerere pictured on January 31, 1985 in Dar es Salam, Tanzania. PHOTO | FILE  NATION MEDIA GROUP "Nadhani hakupaswa Kung'atuka" Nilibahatika kukutana na (BIBI Theresa) ambaye alitem… Read More
  • TQM FOR TANZANIAN EDUCATION QUALITY IMPROVEMENT Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE MicrosoftInternetExplorer4 … Read More
  • SIMBA UJASIRI NDIO SILAHA YETU YA KWELI  Kujitegemea na Kuthamini MASHABIKI ndio MSINGI wa mafanikio ya KWELI ya timu YETU. Lazima tujifunze kuanzia PALE TULIPO. Tuanze na uwezo wetu, ili tuinuke kwa pamoja, WASHABIKI N… Read More
  • "Penye UONGO, UKWELI pia HUJITENGA"Baada ya kuona maswala ya SIASA siyaelewi kabisa (Hasa kwenye mchakato wa katiba), nikaona nifungue kidogo Falsafa na Sayansi ya mambo ya Kisiasa. Nikajifunza mengi tu na kwa kifupi, nikaona kuwa mambo yahusuyo taratibu tuliz… Read More
  • SABUNI BORA TOKA TUKUYU-RUNGWE, TANZANIA.  Photo By Hussein Mjasiriamali AZA HERBAL MEDICATED SOAP. Ni sabuni ya asili iliyotengenezwa kutumia vitu vya asili kama tunda la PARACHICHI. Ndani ya tunda hili kuna maji kiasi kidogo sana ukilinganisha na matu… Read More

0 comments:

Post a Comment